Mtanzania mmoja mmoja. Stori Moja Baada ya Nyingine | Instagram @ mmojammoja | 📸@nsamila

Joined October 2018
87 Photos and videos
😎 It’s the little things that make life beautiful. Magical sunset over Lake Tanganyika.
2
5
62
Katika kikao hiki, wapiga picha wawili @kimaroieca na @nsamila wataonesha picha walizopiga kutoka miradi tofauti ya @voicetweetz nchini Tanzania, kwa madhumuni ya kukuza uelewa mkubwa zaidi wa maendeleo jumuishi - kwa hivyo kujenga ushirikiano wa kweli zaidi. #WikiYaAzaki2019
10
40
”Mimi nikienda kununua nguo nacho zingatia ni kupendeza na kunitosha.” - Kikombo, Dodoma
7
55
".. ni mwaka wa nne toka nihamie hili jiji. Nimepitia mengi ila namshukuru Mungu kwa yote; nimemrudia yeye na amenipa amani. Kuna ambayo najutia. Kuna wakati kwa mfano unakuta mtu humpendi lakini unatembea naye sababu una shida. Sipendi kukumbuka." - (Barabara ya Tisa, Tanga)
2
11
47
"Hakuna uhusiano kati ya Uchagga na ubahili. Mfanyabiashara yeyote anaangalia faida kwa hiyo lazima kuwa makini. Pia hakuna uhusiano kati ya Uchagga na wizi sababu makabila yote wezi, wachawi na bahili wapo. Ila kwa pombe kweli Wachagga tunapenda." -(Goba, Dar Es Salaam)
4
27
184
"Mimi muongeaji sana, tangu ujana. Enzi zangu sikuwa napitwa na jambo, mjuaji kweli hadi nikapewa hilo jina Karedio. Nilikuwa na ndoto ya kuwa msanii ila ndio hivyo maisha si kila ukitamanicho unapata. Mimi maarufu hapa kijijini, hakuna asiyenifahamu."- (Miembeni, Muheza, Tanga)
1
20
150
“Nimefanya hii kazi kwa miaka tisa sasa. Hakuna nywele ngumu kunyoa kama za Wahindi na Waarabu. Hii kazi inanikutanisha na watu wengi. Kuna kero zake. Unaweza kumnyoa mtu hatulii lakini ukimkosea kidogo tu hapakaliki na hapalipiki.”- (Tabata, Dar es Salaam)
3
20
175
Naitwa Buffalo.Nilianza ngumi mwaka 1988. Nimepata mafaniko mengi tu katika ngumi na medali 3 za shaba lakini sitaki mwanangu aje kucheza mchezo huu, ni hatari hasa ukipigwa kichwani. Ngumi sio kama soka, hamko 11, mko wawili,huwezi kutegea na ukijaribu utapigwa ufe.(Tabata, DSM)
11
34
240
Shujaa wangu ni Nelson Mandela. Kaonyesha kutokata tamaa, kupambana hadi kupata unachotaka. Hulka kama hiyo katika maisha sio kitu kidogo wala rahisi. Ushujaa wake pia naupenda kwenye kutaka binadamu waheshimiane bila kujali rangi wala itikadi." - (Kigamboni, Dar Es Salaam)
2
13
106
"Nimerudishwa niende nyumbani kumuita mzazi sababu kuna mwanafunzi nimempiga shuleni ameumia. Kila siku ananitania mimi mapele kutokana na huu upele, na kila nikimwambia mama hafuatilii. Nimemwambia anihamishe shule, hataki. Sina raha shuleni." - (Tangamano, Tanga)
35
40
375
(2/2) "Kinachonisumbua kichwa kiasi sasa hivi ni njia gani nichukue kwenye maisha. Wazazi wangu wanataka nirudi China, ila mimi nafurahia kusafiri na kuifahamu dunia. Kwa hiyo niko hapo katikati, nawaza kuamua kipi cha kufuata." - (Mikocheni, Dar Es Salaam)
8
18
183
(1/2) "Kasumba iko pande zote. Wachina wengi wanadhani kwa kiasi kikubwa Afrika kuna magonjwa tu na umasikini, kitu ambacho si kweli. Watanzania wengi wanadhani kila Mchina anajua Kung Fu na kila bidhaa kutoka China ni feki, na hayo mambo si kweli." -(Mikocheni, Dar Es Salaam)
2
18
172
"Nimejifunza kuwa binadamu tunaishi lakini hatujui kesho yetu. Kikubwa ni kukubali maisha yanabadilika. Nilikuwa na ndoto ya kuwa Mhasibu lakini nikiwa kidato cha 3 nikagundulika kuwa na tatizo ambalo limebadili mwelekeo mzima wa maisha yangu hadi leo." - (Upanga, Dar Es Salaam)
15
70
313
"Ni utamaduni hapa, tunayempenda akitutoka tunachora jina kwenye ukuta wa nyumba. Salah alikuwa mtu poa sana, fundi wa malori ila kuna siku alijiingiza kwenye wizi raia wakamzimisha. Siku anakufa tulikuwa tumetoka msibani na alishiriki hadi kuchimba kaburi."- (Ngarenaro, Arusha)
7
27
287
"Mwanamke kulia ni rahisi. Mara ya mwisho kulia ilikuwa tarehe 4 Januari, birthday yangu. Mama mkwe alikuja kukumbuka usiku kama dakika 3 zimebaki kuingia tarehe 5, akaniletea zawadi muda huo na kunitakia happy birthday. Machozi yalinitoka ya furaha." - (Mikocheni, Dar es Salaam)
8
160
(3/3) "Yule bosi wangu sasa hivi ni dereva wa bodaboda, nikihitaji mizigo toka duka la jumla huwa namtuma. Nimejifunza mambo mengi sana kutokana na matatizo yake. Ukiwa kijana ni bora kujiweka karibu na watu kuliko kujifanya wewe ndio kila kitu." - (Tabata, Dar Es Salaam)
4
19
180
(2/3) "Ilitokea siku bosi wangu alichukua gari la mtu akalewa akagonga ikatakiwa alipe. Pesa hakuwa nayo kwa hiyo ikabidi kuliuza duka, ikabidi mimi niondoke na akiba yangu nilikuwa natunza nikafungua kibanda na kuanza kidogo kidogo mpaka kufikia hapa." - (Tabata, Dar Es Salaam)
4
17
127
(1/3) "Nimeanza kufanya hii biashara ya duka mwaka 2011, nina mipango mingi sana na najiona nina deni kubwa sana katika maisha yangu. Nilianza kufanya kazi kwenye duka la rafiki yangu ila kuna mambo yalitokea yakabadili mwelekeo wa maisha." - (Tabata, Dar Es Salaam)
1
14
101
"Namshukuru mamangu kwa malezi mpaka hapa. Niko Chuo Kikuu nasomea Saikolojia na Mahusiano ya Kimataifa. Nasomea Saikolojia kwa sababu naona ni tatizo kubwa sana katika jamii ya Watanzania, nadhani ninaweza kutatua kitu fulani kwenye jamii yangu." - (Kigamboni, Dar Es Salaam)
7
28
271
"Ndoto zangu bado hazijatimia. Najiona bado nipo usingizini. Napenda kusaidia mwanadamu yeyote anayetaabika. Naomba siku dongo (pesa) limenidondokea la maana nijenge kituo cha afya kwa ajili ya watu wasiojiweza. Bado tuko hai. Hii ndoto itatimia."- (Chalagule, Morogoro)
6
33
262