Mama Samia, pengine wanaokuzunguka wanakudanganya sana. Na msingi wa uongo huo kwao unaweza kuwa biashara kubwa sana. Wanaweza kuwa wanatumia intimidation kama strategy muhimu kwa maslahi yao. Lakini ukweli ni kwamba siasa za aina hii za kuongeza presha na taharuki hazileti faida ya muda mrefu kwa nchi, bali kwa watu wachache tu wanaonufaika na hali hiyo.
Kuhusu Mh Tundu Lissu, kumuweka mahabusu au kumdhibiti kisiasa hakutaondoa changamoto za kisiasa, bali kunaendelea kuongeza taharuki zaidi ndani na nje ya nchi. Hasara kubwa si yeye kufanya siasa akiwa nje, bali ni kuendelea kumuweka mahabusu.
Kwa mtazamo huu, hii sio faida , bali inaweza kuwa faida kwa watu wanaonufaika na mvutano huu. Ndiyo maana wakati mwingine huonekana kuna mkakati wa kupandisha presha ili maslahi fulani yaendelee kunufaika. Hofu nayo ni biashara , tena Tax free.