VIDEO:
Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mbeya, Masaga Kaloli, ameingilia kati mjadala mzito wa kisiasa uliozuka bungeni hivi karibuni baada ya Mbunge wa Tunguu (Zanzibar), Simai Mohammed Said, kambatiza kiongozifulani serikali jina la "Yuda Iskariote."
Akizungumza na wananchi mkoani Mbeya jana Jumapili, Juni 7, 2026, Kaloli amesema kuwa CHADEMA haitaki kuingilia migogoro ya ndani ya chama tawala, lakini akatoa ofa kwa kiongozi huyo anayeitwa Yuda kwamba kama ana nia njema na nchi basi anakaribishwa kujiunga na upinzani.
Kaloli ametumia sakata hilo kukosoa mfumo wa uwakilishi wa wabunge wa chama tawala bungeni, akidai kuwa wameacha wajibu wao wa kikatiba wa kuisimamia serikali na kutetea wananchi, na badala yake wamebaki kumsifu na kumlinda mkuu wa nchi pekee.