Tuimalizie sasa 🤦🏽♀️
Wakati anajiandaa akampigia, akamwambia "mama utake, usitake mimi naondoka, huyu kaka ni mchawi, mpaka nife mama yangu? Kama hautanipokea nyumbani basi"
Mama yake akamsihi asubiri aende kumchukua na gari, binti akakubali.
Baada ya muda mama akaja akiwa na mama mdogo (mdogo wa mama) wakamchukua na kwenda nae kwa mama nyumbani.
Jioni jamaa anapiga simu, mbona mlango umefungwa upo wapi, binti ndo akamwambia ameondoka yupo home anajiuguza atarudi akishapona na kwamba funguo zipo juu ya mlango.
Jamaa akaanza kufoka kwann ameondoka na kumrushia threats mama yake kwa kumchukua mkewe bila kumuaga. Lakini ajabu hakuongelea kuhusu mkongojo hata kidogo.
Siku mbili zikapita bila vurugu zozote ila tukumbuke kuwa binti alikuwa bado anajiuguza mshono kwa kujifungua sababu ni siku 4 tu toka afanyiwe upasuaji..,
Basi jamaa akaenda kumtembelea hiyo siku. Binti alivyosikia jamaa kaja, hakutoka kumuona, alikataa kabisa.
Jamaa akakaa nje anamuongelesha mtoto wa mama yake mdogo mwenye miaka kama 6 hivi. Baada ya muda akaondoka.
Muda kidogo, binti akatoka nje kupunga upepo akamuona yule mtoto anachezea mpira. Mpira unafanana na mipira ya kufuma ile ya mtaani. Dogo akamwambia uncle amenipa huu mpira.
Mmh binti moyo wake ukakataa, akamwambia dogo naomba niuone.
Akaingia ndani akachukua kisu akaukata katikati akakuta kuna Umbilical Cord ya mtoto yote kama ilivyo. (hii nimeona picha yake kwa macho yangu)
Akamuita mama yake na kulia sana na hapo ndo ilikuwa mwisho wa uvumilivu wake.
Akawaita kikao watu wazima na masheikh, na jamaa akaitwa, binti akaelezea yote., Baada ya kumbana sana Jamaa akaambiwa aelezee, akasema
- Alitakiwa kutoa sacrifice ya mtoto wa kwanza wa binti wa kwanza. (mzaliwa wa kwanza) lkn hakutakiwa kumuoa na hayo ndio makosa aliyoyafanya kwenye mashart yake.
-Umbilical cord ni ya mtoto wake yule aliyepewa akamzike.
-Mafanikio yake yalikuwa yanategemea nyota ya mkewe.
Ingawa jamaa aliomba msamaha sana but binti hakumsamehe na kuomba talaka.
Ni mwaka wa pili sasa, Jamaa mpaka leo amekataa kutoa talaka, lakini binti yupo kwao anaendelea na maisha yake na kwa sasa ni mjasiriamali mzuri tu kasema anapanga siku aende mahakamani kuomba talaka ya serikalini.
Upande wa pili jamaa hana biashara tena, zile safari, magari na pesa hamna.
Limebaki jina tu. Bado anafanya biashara lakini si kwa ukubwa kama ilivyokuwa awali. Anasema bado anamtaka mkewe arudi.
Mwisho.