Tiba pekee ya kutibu watanzania kwasasa ni yafuatayo.
1. UWAJIBIKAJI kwa jeshi zima la polisi. Hapa tutaanza na BILIONEA WAMBURA, MURILO ,Bila kumsahau JAMBAZI KUU MAFWELE na kibaka msaidizi “GEORGE”.
2. UCHAGUZI URUDIWE. Hawa wanaoitwa viongizi wa serikali wa sasa HATUWATAMBUI na hizo nafasi walizonazo zina damu za watanzania wasio na HATIA. Lazima tupate viongozi wanaotokana na wananchi.
3. TUPATE KATIBA MPYA. Mzizi wa tatizo wa hii nchi ni katiba MBOVU iliyoundwa na watu wanne miaka ya TISINI. Leo hii zaidi ya asilimia 70 ya nchi ni vijana ambao HATUKUWEPO-ndiomaana madudu ni mengi.
4. WATANZANIA WAPEWE MIILI YA NDUGU ZAO WAZIKE. Mpaka leo familia nyingi kwa maelfu HAZIJAZIKA wapendwa wao baada ya mauaji ya kikatili yaliyoongozwa na vyombo vya usalama. Ushahidi upo kwa maelfu wakitekeleza hayo mauji. Msiba hauishi mpaka watu wazike hiyo ndio TAMADUNI YETU.
5. WATANZANIA WALIPWE FIDIA. Waathirika wote wa MAAMDAMANO ya MO 29 lazima walipwe fidia. Familia ni nyingi sana zimeathirika na yale mauaji, lazima watu wafidiwe hata kwa kidogo ili tuone nia ya kutaka kuweka mambo sawa.
KITU KINAITWA “MARIDHIANO” huu ni mradi ambao hautakiwi hata kujadiliwa na watu wenye akili timamu. Unataka maridhiano ya nani na nani?
Mimi binafsi naamini wanaotakiwa kukaa meza ya maridhiano ni wale wahanga wa MO29 ambao wengi wamekufa , wengine wamepata vilema na wengine wametekwa mpaka leo hatujui walipo.
Hakuna CHAMA au mtu anayo haki ya kukaa meza ya MARIDHIANO labda kama anabiashara zake-kukubali maridhiano ni kutumia VIFO VYA NDUGU ZETU KUJINUFAISHA. HATUTAKUBALI—TUTASHUGHULIKA NA WEWE BILA KUKUONEA AIBU.
TUTAKUWEPO🫵🏾😎