Swahiba ashiriki uzinduzi wa Sera ya Mambo ya Nje.
Benki ya CRDB imeshiriki katika uzinduzi wa Sera ya Mambo ya Nje ya mwaka 2001, toleo jipya la mwaka 2024, uliofanyika jijini Dar es Salaam na kuongozwa na mgeni rasm Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na Mh. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
Tukiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Bi Azmina Hemed, pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Biashara, Bw. Jacob Nangi na timu ya wafanyakazi kutoka benki, kama mdau mkubwa wa maendeleo na fursa za uchumi ndani na nje ya nchi, Benki yetu inaunga mkono hatua hii kubwa ya kisera na itaendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Mambo ya Nje katika kila eneo muhimu ili kutekeleza malengo ya sera hii kwa manufaa ya taifa letu.
Katika kuunga mkono kauli mbiu, Dunia ni Fursa! Miaka 30 ya Benki ya CRDB ni mfano wa kuigwa kama Benki ya kwanza kukamata fursa nje ya nchi na kutanua mbawa za huduma za kibenki nchini Burundi, Congo, na sasa tunajiandaa kufungua fursa mpya Dubai, huku tukiendelea kuangazia fursa zaidi barani Afrika, kama visiwa vya Komoro na Zambia, kwa kuzingatia mwelekeo wa maono ya serikali yetu. Lakini pia, benki yetu imeboresha mchakato wa kufungua akaunti kwa Watanzania wote, wakiwemo wanaoishi nje ya nchi (Diaspora), ambapo kwa sasa wanaweza kufungua akaunti zao wenyewe kupitia programu ya SimBanking huku tukihakikisha tumewaondolea adha ya ada za kila mwezi.
Tukiwa kama Benki kiongozi, tunaendelea kushirikiana na Serikali na taasisi binafsi kusukuma grudumu la maendelo ndani na nje ya nchi
#CRDBBank #DuniaNiFursa #tunakusikiliza