Filter
Exclude
Time range
-
Near
“Nimeona pia kwenye Mitandao baadhi ya Watu wanatamani kuleta chokochoko kwenye Mikoa yetu, na kwa bahati mbaya sana nguvu inayotumika katika kulinda amani wakati mwingine inakuwa ya kawaida sana, nguvu zitakazoendelea kutumika kulinda amani pengine haijawahi kutokea wala kuonwa katika kipindi chote, na pengine kuna wengine wanadhani kuna nguvu ishawahi kutumika mahali, kwenye kikao hiki nataka niwathibitishie yalikuwa ni majaribio kutumia nguvu kulinda amani.” Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila akizungumza hii leo na Wenyeviti na Watendaji wa Mitaa na Kata kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere. #KitengeUpdates
27
5
80
11,188
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametangaza kuwa Jumatano, tarehe 17 Juni 2026, itakuwa siku ya mapumziko kwa Zanzibar ili kuukaribisha Mwaka Mpya wa Kiislamu 1448 Hijria. Rais Dkt. Mwinyi ametoa tamko hilo leo, tarehe 15 Juni 2026, Ikulu Zanzibar, ikiwa ni utekelezaji wa uamuzi wa Serikali wa kuutambua Mwaka Mpya wa Kiislamu kuwa miongoni mwa siku muhimu Zanzibar. Amesema siku hiyo itatoa fursa kwa Wananchi, hususan waumini wa dini ya Kiislamu, kuukarıbısha mwaka mpya kwa ibada, dua, na matendo mema, pamoja na kumuomba Mwenyezi Mungu aendelee kuijaalia Zanzibar na Tanzania kwa ujumla amani, umoja na ustawi. Alhaj Dkt. Mwinyi amewataka Wananchi kuutumia mwaka mpya huo kujitathmini, kuimarisha uchamungu, kusaidiana na kuendeleza maadili mema yanayojenga familia na Taifa lenye mshikamano. Aidha, amezitaka taasisi za Serikali, taasisi binafsi, waajiri na Wananchi wote kuzingatia tangazo hilo kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa. Rais Dkt. Mwinyi amewatakia Waislamu na wananchi wote heri ya Mwaka Mpya wa Kiislamu 1448 Hijria, akimuomba Mwenyezi Mungu aufanye kuwa mwaka wa kheri, amani, afya njema na maendeleo kwa wote. #KitengeUpdates
3
45
1,703
Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limekanusha taarifa kuhusiana na picha mjongeo iliyochapishwa katika Mtandao wa Kijamii na mtu aitwaye Maria Sarungi akieleza kuwa Polisi amepigika Arusha. Akitoa taarifa hiyo leo Juni 14, 2026 Kamanda wa Polisi Mkoani humo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Justine Masejo amesema taarifa hiyo ni ya uongo kwani Mkoani Arusha hakuna tukio lolote lililotokea kuhusiana na Askari kupigwa. SACP Masejo amebainisha kuwa inaonesha wazi kuwa picha mjongeo hiyo ilichukuliwa maeneo mengine nje ya nchi na kisha kutengenezewa maneno ya uongo. Aidha, amewaomba Wananchi kupuuza taarifa hiyo, kwani mtu huyo amekuwa akiandaa na kusambaza maudhui ya uongo, uchonganishi na kutaka kuleta taharuki kwa jamii jambo ambalo ni kinyume na makuzi, mila, desturi na mifumo ya kisheria. Jeshi la Polisi mkoani humo, limeendelea kutoa wito na onyo kwa baadhi ya watu wenye tabia kama hizo za kuandaa na kusambaza taarifa za uongo, kupandikiza chuki na kuchonganisha jamii kuacha kufanya hivyo kwani ni kinyume cha sheria. #KitengeUpdates
2
1
52
8,183
Juni 14 kila mwaka ni siku ya kuzaliwa kwa Rais wa Marekani, Donald Trump aliyezaliwa mnamo Juni 14, 1946 na leo anatimiza miaka 80. Licha ya umri huo, Rais huyo wa 45 na 47 wa Taifa la Marekani anaendelea kuwa na shughuli nyingi sana katika Siasa na Biashara bila kuonesha dalili za kuchoka. Happy 80th Birthday, President Donald Trump #KitengeUpdates
2
9
152
6,677
Filbert Philimon (23), Mwanachuo wa Chuo Kikuu cha St. John’s anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma kwa kuhusika katika tukio la kuchoma Chumba moto na kusababisha Vifo vya Watu wawili (Rebeka James na Felister Peter) katika Mtaa wa Kikuyu Dodoma mjini mnamo Juni 6, 2026 majira ya saa nane usiku. Taarifa ya leo Juni 14 2026 iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma imeeleza kuwa baada ya tukio hilo la uhalifu kutendeka, Jeshi hilo lilifanya uchunguzi wa haraka na wenye umahiri wa hali ya juu uliofanikisha kubainisha kuwa tukio hili limetendwa na Mtuhumiwa huyo. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Juni 13, 2026 Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma lilimkamata Mtuhumiwa huyo katika stendi ya mabasi ya Magufuli Jijini Dar es Salaam akiwa katika harakati za kuukimbia mkono wa Sheria. Aidha Mtuhumiwa amekiri kutenda kosa hilo Kwa kutumia Mafuta ya Petrol lita mbili sababu kubwa ikiwa ni wivu wa mapenzi baada ya kuachwa na Mpenzi wake Marehemu Felister Peter Francis ambaye alimpata Mwanaume mwingine. Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma limetoa wito na kuwaasa Wananchi na Wana-Vyuo wa Elimu ya juu kuacha kujiingiza kwenye vitendo vya kihalifu kama ilivyo katika tukio hilo huku likiwasihi Wanavyuo kuendelea na masomo yao ipasavyo na watafute msaada wa kisaikolojia na kutembelea washauri nasihi ili kukabiliana na msongo wa mawazo. #KitengeUpdates
3
3
83
8,153
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea mradi wa Uwanja wa AFCON Fumba kwa ajili ya kukagua maendeleo ya ujenzi wake. Ziara hiyo ya ukaguzi imefanyika leo, tarehe 14 Juni 2026, ambapo Rais Dkt. Mwinyi ametembelea maeneo mbalimbali ya uwanja huo wa kisasa unaojengwa na Kampuni ya Orkun Group ya Uturuki unaotarajiwa kutumika katika Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2027. Rais Dkt. Mwinyi ameendelea na utaratibu wake wa kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Nchi tatu za Afrika Mashariki, Tanzania, Kenya na Uganda, zinatarajiwa kuandaa kwa pamoja Michuano ya AFCON 2027. Uwanja wa AFCON Fumba ni miongoni mwa viwanja vinavyotarajiwa kutumika katika michuano hiyo. #KitengeUpdates
41
2,450
Morocco imetangaza kuwa haitawasilisha tena maombi ya kuandaa Mashindano ya soka ya Afrika, ikielekeza nguvu zake katika maandalizi ya matukio makubwa ya kimataifa yanayotarajiwa kufanyika katika miaka ijayo. Rais wa Shirikisho la soka la Morocco, Fouzi Lekjaa, amesema nchi hiyo sasa itaelekeza rasilimali zake za kiutawala, kifedha na Miundombinu katika Maandalizi ya 2029 FIFA Club World Cup na 2030 FIFA World Cup. Morocco itakuwa mwenyeji mwenza wa Kombe la Dunia 2030 pamoja na Hispania na Ureno, hatua ambayo itaifanya kuwa nchi ya kwanza ya Afrika Kaskazini kuandaa Mashindano hayo makubwa ya soka duniani. Kwa miaka ya hivi karibuni, Morocco imekuwa miongoni mwa mataifa yaliyoandaa mara kwa mara Mashindano ya soka ya Afrika na kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika Viwanja vya Michezo, usafiri na Miundombinu mingine ya michezo. Hata hivyo, viongozi wa soka nchini humo wanaamini kuwa ukubwa wa majukumu yanayokuja unahitaji umakini wa hali ya juu ili kuhakikisha maandalizi ya mashindano hayo ya kimataifa yanafanyika kwa mafanikio. #KitengeUpdates
21
11
590
45,569
Meya wa Manispaa ya San Miguel Amatitlán Kusini mwa Mexico ameuawa kwa kupigwa risasi, katika eneo linalokumbwa na shughuli za makundi ya biashara haramu ya dawa za kulevya. Kwa mujibu wa Ofisi ya Mwendesha Mashtaka ya Jimbo la Oaxaca, Meya huyo, Joel Ángel Bravo Martínez, alikuwa mwathirika wa shambulio la kutumia silaha za moto. Vyombo vya habari vya eneo hilo vimeripoti kuwa watu wenye silaha walimvamia Nyumbani kwake na kumpiga risasi na kusababisha kifo chake. Mamlaka zimeanzisha uchunguzi ili kubaini waliohusika na sababu za mauaji hayo. Tukio hilo linaongeza wasiwasi kuhusu usalama wa Viongozi wa kisiasa katika baadhi ya maeneo ya Mexico yanayokabiliwa na ushawishi mkubwa wa magenge ya uhalifu na biashara ya dawa za kulevya. Hadi sasa, hakuna kundi lililodai kuhusika na mauaji hayo, huku uchunguzi ukiendelea. #KitengeUpdates
2
4
76
9,399
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dodoma, Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Ndugu Kenani Laban Kihongosi, amesema kuwa zipo taarifa zinazodai kuwepo kwa watu wanaojaribu kuchochea migawanyiko na vurugu zinazoweza kuhatarisha amani na utulivu wa Taifa. Kihongosi ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kusimama imara kulinda uhuru, umoja na mshikamano wa nchi yetu, huku akisisitiza umuhimu wa kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuimarisha umoja wa kitaifa, amani na maendeleo ya Watanzania wote. #KitengeUpdates
2
10
1,705
Televisheni ya taifa ya Iran imetangaza kuwa Mazishi ya aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei, yatafanyika tarehe 9 Julai katika Mji wa Mashhad. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, shughuli za kuaga Mwili na Maombolezo zitaanza tarehe 4 Julai mjini Tehran kabla ya kuendelea katika Miji mingine ya Kidini ya Qom na Mashhad. Mazishi ya mwisho yatafanyika tarehe 9 Julai katika eneo la Kaburi la Imam Reza Shrine. Khamenei alifariki mwezi Februari 2026, akimaliza zaidi ya miongo mitatu akiwa Kiongozi wa juu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Serikali ya Iran inatarajia Mamilioni ya waombolezaji kushiriki katika shughuli hizo za kitaifa. Tangazo hilo linakuja baada ya kuahirishwa mara kadhaa kwa mazishi hayo kutokana na hali ya usalama na maandalizi ya hafla hiyo kubwa, ambayo inatarajiwa kuwa miongoni mwa mazishi makubwa zaidi katika historia ya Iran. #KitengeUpdates
2
3
31
2,604
Kampuni inayokuja kasi ya uuzaji Magari makubwa ya biashara (Malori) Six Continental Group, imetangazwa kuwa ndiyo Kampuni bora ya uagizaji Magari ya Baishara na kukabidhiwa Tuzo. Tuzo hiyo ya heshima kubwa imetolewa kwao katika Tuzo za Kampuni Bora za Mwaka Afrika za ACOYA 2026. Katika taarifa ya kushukuru Tuzo hiyo, Kampuni hiyo imesema, Mafanikio hayo yametokana na wateja wao, washirika wao, na timu yao nzima yenye kujitolea, ambao wanaamini msaada huo umeendelea kuchochea mafanikio yao. Ubora. Uaminifu. Maendeleo. 🚛🏆 #KitengeUpdates
1
18
1,262
Binadamu mwenye ukwasi (utajiri) mkubwa zaidi duniani kwa sasa, mfanyabiashara Elon Musk ametangazwa kuwa Mtu wa kwanza duniani kufikia utajiri wa dola za Marekani Trilioni moja kufuatia hisa za Kampuni yake ya SpaceX kuanza kuuzwa katika soko la hisa la Nasdaq. Ripoti ya Jarida la Forbes iliyotolewa leo June 12, 2026 imeeleza kuwa hisa za SpaceX zimeanza kuuzwa kwa dola 150 kwa kila hisa, jambo lililoifanya Kampuni hiyo kufikia thamani ya karibu dola Trilioni mbili sokoni ambapo hatua hiyo imeongeza utajiri wa Mmiliki huyo wa Kampuni za SpaceX, Tesla na Mtandao wa X kufikia takribani dola Trilioni 1.1 hadi kufikia Ijumaa ya leo. Aidha ripoti hiyo imeeleza mpaka kufikia Alhamisi jioni utajiri wa Musk ulikuwa umeongezeka kwa dola bilioni 188 na kufikia dola bilioni 982 baada ya SpaceX kupanga bei ya awali ya hisa zake kuwa dola 135 kwa kila hisa ambapo Musk anamiliki hisa bilioni 4.8 za SpaceX zenye thamani ya dola bilioni 715 pamoja na haki za kununua hisa nyingine Milioni 350 zenye thamani ya dola bilioni 50, hali inayompa umiliki wa asilimia 38 wa Kampuni hiyo. #KitengeUpdates
3
4
99
5,165
Kiungo wa kati wa Black Stars, Thomas Partey, hatashiriki katika mechi ya ufunguzi ya timu hiyo dhidi ya Panama kwenye michuano ya 2026 FIFA World Cup baada ya kuripotiwa kunyimwa ruhusa ya kuingia nchini Canada. Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana, Partey alikumbwa na changamoto za kiutawala zilizomzuia kuingia Canada, hali iliyomfanya ashindwe kujiunga na kikosi cha Black Stars kwa wakati kabla ya mchezo huo muhimu wa ufunguzi. Kutokuwepo kwa nyota huyo kunatajwa kuwa pigo kubwa kwa Black Stars, kwani amekuwa mmoja wa wachezaji muhimu katika safu ya kiungo ya timu hiyo kutokana na uzoefu wake wa kimataifa na uwezo wake wa kudhibiti mchezo katikati ya uwanja. Benchi la ufundi la Black Stars sasa linalazimika kufanya marekebisho ya kikosi ili kuziba pengo la Partey huku timu ikijiandaa kukabiliana na Panama katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa. Mashabiki wa Ghana wameonyesha masikitiko yao kufuatia taarifa hizo, wakitumaini kuwa suala hilo litapatiwa ufumbuzi haraka ili Partey aweze kujiunga na timu kwa michezo inayofuata ya mashindano hayo. Black Stars ina matumaini ya kuanza vyema kampeni yake ya Kombe la Dunia 2026 licha ya kukosekana kwa mmoja wa wachezaji wake tegemeo katika mchezo wa kwanza. #KitengeUpdates
2
90
5,267
Kiongozi wa upinzani nchini DR Congo, Martin Fayulu, alijeruhiwa Ijumaa wakati wa Maandamano yaliyofanyika karibu na Jengo la Bunge la Taifa mjini Kinshasa. Maandamano hayo yaliyoandaliwa na Vyama vya upinzani yalizuiwa na Polisi baada ya Mamlaka kupiga marufuku mikusanyiko karibu na Jengo la Bunge. Hali hiyo ilisababisha vurugu kati ya Waandamanaji na vikosi vya usalama. Picha na video zilizosambazwa kwenye Mitandao ya kijamii zilimuonyesha Fayulu akiwa na damu kwenye nguo zake huku akisaidiwa kuondoka eneo la tukio na wafuasi wake. Kufikia sasa, ukubwa wa majeraha yake haujatangazwa rasmi. Mamlaka za Kinshasa zilikuwa zimewaelekeza Waandamanaji kufanya mkutano wao katika eneo la Kasa-Vubu badala ya kuandamana karibu na Bunge, lakini upinzani uliendelea na Maandamano hayo. Maandamano hayo yanajiri siku chache baada ya Bunge la Taifa kupitisha muswada wa sheria ya kura ya maoni. Muswada huo sasa unasubiri kujadiliwa na Seneti kabla ya kutiwa saini na Rais Félix Tshisekedi. #KitengeUpdates
1
3
48
10,033
Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama barabarani Mkoani Arusha limeendelea kuimarisha mikakati ya kuzuia ajali za barabarani kwa kukutana na Mawakala wa Mabasi wanaotoa huduma za usafiri wa abiria ndani na nje ya Mkoa huo. Akizungumza mara baada ya Kikao hicho leo, Mkuu wa Kikosi hicho Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Zauda Mohamed amesema wamekutana na Mawakala hao kuhakikisha sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani zinazingatiwa wakati wote. ACP Zauda amebainisha kuwa kutokana na uwepo wa vituo vya mabasi maeneo mbalimbali mkoani humo, kupitia kikao hicho wameweka mpangokazi mzuri wa kukagua Mabasi hayo pamoja na Madereva kabla ya kuanza safari. #KitengeUpdates
1
16
2,382
Rais wa zamani wa Jamhuriy ya Kidemokrasia ya Congo, Joseph Kabila, ametoa onyo kali kwa Rais Félix Tshisekedi kuhusu mpango unaodaiwa wa kubadili Katiba ya nchi hiyo. Katika ujumbe wake, Kabila amesema hali ni ya hatari na kwamba Mamlaka za sasa zinaonekana kusukuma mbele mabadiliko ya kikatiba ambayo, kwa maoni yake, yanaweza kuhatarisha demokrasia na mfumo wa kubadilishana madaraka kwa njia ya uchaguzi. Akinukuu kifungu cha 64 cha Katiba ya DR Congo, Kabila amesema Wananchi wana haki ya kulinda taifa na katiba yake dhidi ya kile alichokiita ukiukwaji wa misingi ya kikatiba. Amesisitiza kuwa hakuna mtu atakayepaswa kudai baadaye kwamba hakufahamu kilichokuwa kinaendelea. Kabila pia ametoa wito kwa jumuiya ya Kimataifa na Wananchi wa Congo kufuatilia kwa karibu maendeleo ya kisiasa nchini humo. Kwa mujibu wake, hatua yoyote ya kubadili Katiba kwa maslahi ya kisiasa inaweza kuimarisha utawala usio na mipaka, kudhoofisha taasisi za kidemokrasia na kuzuia uwezekano wa mabadiliko ya Uongozi kupitia uchaguzi. #KitengeUpdates
5
3
129
14,053
Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro, limetoa angalizo katika kipindi chote cha Michuano ya Kombe la Dunia 2026 kwa michezo yenye ratiba za usiku Watoto wadhibitiwe kwenda kwenye kumbi na vibanda umiza, likisisitiza kuimarisha ulinzi na usalama maeneo yote yatakayokuwa yakionyesha Mashindano hayo. Kamanda wa Mkoa wa Morogoro, ACP Andrew Kantimbo ametoa angalizo hilo wakati akitoa ufafanuzi kwa Waandishi wa habari mkoani humo jinsi Jeshi hilo lilivyojipanga kuimarisha usalama katika kwa Mashabiki wa soka watakaofuatilia Mashindano hayo kwenye kumbi na vibanda umiza kwenye maeneo mbalimbali ya mkoa huo. #KitengeUpdates
2
2
21
1,442
Six Continental Group (@sixcontinentalgroup), imemtangaza CPA Benson Mahenya kuwa Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Kundi (Group Chief Executive Officer - Group CEO). Uteuzi huo unaashiria mwanzo wa awamu mpya ya Uongozi wa kimkakati katika Kampuni hiyo inayokua kwa kasi katika sekta za usafirishaji, vifaa (logistics) na biashara barani Afrika. Mahenya ni Kiongozi mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 30 katika sekta za Benki, Fedha, Viwanda, ushauri wa Biashara, utawala wa mashirika na Uongozi wa Kampuni. Amejijengea sifa kubwa nchini Tanzania kutokana na uwezo wake wa kuongoza mabadiliko ya kimkakati na kuimarisha utendaji wa taasisi mbalimbali. Katika nafasi yake mpya, anatarajiwa kuongoza juhudi za Six Continental Group katika kuendeleza ukuaji wa biashara, kupanua shughuli zake katika Masoko ya Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika, pamoja na kuimarisha nafasi ya Kampuni katika sekta ya usafirishaji na Biashara ya vifaa vya usafiri. Uteuzi wake unaonyesha dhamira ya Six Continental Group ya kuendelea kuimarisha uongozi wake na kufanikisha malengo ya muda mrefu ya ukuaji na ushindani katika soko la Afrika. #KitengeUpdates
2
4
42
7,059
Maafisa watano wa Polisi wameuawa na wengine watano kujeruhiwa katika shambulio la watu wenye silaha lililotokea Jumatano katika Jimbo la Michoacán Magharibi mwa Mexico, eneo linalokumbwa na shughuli za magenge ya biashara ya dawa za kulevya. Kwa mujibu wa Mamlaka za eneo hilo, Polisi hao walishambuliwa walipokuwa wakisafiri katika gari lao katika Manispaa ya Nahuatzen. Picha zilizochapishwa zinaonyesha gari hilo likiwa na mashimo mengi ya risasi kutokana na mashambulizi hayo. Tukio hilo limetokea saa chache kabla ya kuanza kwa kombe la Dunia 2026, ambalo linaandaliwa kwa pamoja na Mexico, Marekani na Canada. Mamlaka za Mexico zimeanzisha uchunguzi wa shambulio hilo huku juhudi za kuwasaka waliohusika zikiendelea. Serikali imeahidi kuimarisha usalama katika maeneo mbalimbali ya nchi wakati wa kipindi cha mashindano ya Kombe la Dunia. #KitengeUpdates
6
4
99
11,310
Jeshi la Marekani limeanzisha mashambulizi dhidi ya maeneo kadhaa nchini Iran, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamandi Kuu ya Marekani (CENTCOM). Marekani imesema operesheni hiyo ni jibu kwa kile ilichokiita uchokozi wa Iran ambao umeendelea kwa muda. Katika hatua inayoongeza mvutano katika eneo la Mashariki ya Kati, Rais wa Marekani, Donald Trump, alionya kwamba nchi yake iko tayari kuendelea na mashambulizi zaidi ikiwa hakutakuwa na maendeleo ya haraka katika mazungumzo ya kutafuta suluhisho la mgogoro huo. Akizungumza kuhusu hali hiyo, Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Pete Hegseth, alisema Kamandi Kuu ya Marekani imepewa jukumu la kuendelea na operesheni zake kwa nguvu, akisisitiza kuwa Marekani itachukua hatua kali dhidi ya Iran kama ilivyoelekezwa na Rais. Hata hivyo, pamoja na ongezeko la shughuli za kijeshi, juhudi za kidiplomasia bado zinaendelea. Trump amesema Iran inaweza kufikia makubaliano na Marekani ikiwa itakubali kusaini mkataba unaojadiliwa kwa sasa. #KitengeUpdates
1
64
4,622