Mkazi wa Tabata jijini Dar es Salaam,
Victoria Mkwizu amejifungua pacha watano ambapo wa kiume ni watatu na wawili wa kike.
Victoria amejifungua watoto hao Jumamosi ya Juni 13, 2026 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam.
Taarifa ya MNH imesema jopo la madaktari bingwa wamefanikisha kujifungua salama kwa Victoria.
"Watoto hao, watatu wa kiume na wawili wa kike, wamezaliwa wakiwa katika hali nzuri na wanaendelea kupatiwa uangalizi wa karibu, huku Muhimbili ikiendelea kusimamia huduma bora kwa mama na watoto hao," imeeleza taarifa ya MNH.
#mwananchiupdates
#tunawezeshataifa