Ukienda kutafuta fursa mahali, usijiandae kuelezea tu ulichosoma. Jiandae kuelezea unachoweza kufanya.
Na ukiulizwa unatafuta kazi gani, epuka kusema ‘yoyote itanifaa’. Jibu la namna hiyo humfanya mtu ashindwe kuona au kufahamu thamani yako.
Badala yake sema, ‘Nina ujuzi katika maeneo A, B na C. Pia ninaweza kujifunza kwa haraka na nina uwezo wa kuendana na mazingira tofauti ya kazi. Naweza kufanya kazi zinazohusiana na xyz, lakini pia nipo tayari kusikiliza ushauri wako kuhusu eneo ambalo unaweza kuona ninafaa zaidi.’
Hapo unakuwa hujauza vyeti au kile kinaitwa elimu pekee. Umeuza uwezo wako, namna unavyofikiri, na utayari wako wa kukua.
Watu wengi wanatafuta kazi. Wachache wanajua namna ya kujieleza kusikoacha shaka kwa anayesikiliza.