Mm ninae Bukoba, niko dar naomba mnichangie basi
Masela kwenye ujinga huwa tunapeana sapoti kubwa sana😂🙌.
Nakumbuka kuna mwanetu mmoja enzi tupo chuo alimtongoza manzi karbu miezi 6 anabembeleza tu,.
Kipindi cha likizo ile ndefu ya mwezi wa 8 hadi wa 10, . manzi akamkubalia mwana, na mwana kwao Iringa then manzi kwao ni mwanza,.. Wasiwasi wa mchizi ni kusubiri hadi chuo kifunguliwe anaweza akatemwa tena,.. bhasi akatuomba tumchangie nauli aende mwanza, kwenye ujinga tena, chap tu tukamchangia mwanetu, kwenye uwanja wa ugenini akatuwakilishe vyema😂🔥, sharti lilikuwa picha tu akiwa na mchumba🙌.