Takwimu za Wizara ya Mambo ya Ndani, Jeshi la Polisi zinaonesha ukatili wa kingono kwa jinsia zote umeshuka kutoka matukio 12,749 mwaka 2024 hadi 11,625 mwaka 2025. Hayo yameelezwa leo na Dkt. Dorothy Gwajima, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.