Naungana na watanzania wote wenye upendo wa dhati na nchi yao, kutoa pole kwa familia, ndugu, na marafiki wa wote waliopoteza maisha au kujeruhiwa katika maandamano yaliyofanyika siku ya uchaguzi October 29.
Ni huzuni kubwa kuona damu ya Watanzania ikimwagika katika kipindi ambacho tunapaswa kutumia sauti na busara kujenga demokrasia yetu. Maisha ya kila mtanzania ni yenye thamani, na kila tone la damu lililomwagika litukumbushe kuwa haki, amani, umoja na mazungumzo ya kijamii ni msingi wa taifa letu.
Kwa heshima tunaomba mamlaka husika kuchukua hatua za haki na za kibinadamu kuhakikisha ukweli unajulikana, wahusika wanawajibishwa na haki inatendeka bila upendeleo.
Kwa familia zilizoathirika, tuko nanyi katika maombi, huruma na matumaini. Mungu awafariji, na taifa letu lijifunze kuthamini uhai na utu zaidi ya tofauti zetu za kisiasa.
Taifa lenye amani ni taifa linalokubali ukweli, hata pale ukweli huo unauma. MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE.