MAMBO YA UZAWA YA AFRIKA KUSINI YAMEPANGA KUFANYIKA ZANZIBAR
Naibu Waziri wa AJIRA amesema Zanzibar kuanza kufukuza Watanganyika wanaofanya kazi visiwani upo kwa hoja kwamba sio wazawa wa Zanzibar
Amesema wakipitishiwa bajeti ya wizara yake, watachukua hatua zinayofanana na zile za Afrika Kusini kuondoa wasio wazaliwa wa Zanzibar kwenye ajira na kupeleka ajira hizo kwa Wazanzibar bila kuja vigezo vya uzoefu au kitaalumu kuhusu ajira zilizotangazwa, Tanganyika na Zanzibar hazina sheria inayoweka vizuizi vya ajira kwa mzawa wa upande wowote ule, amesema atahakikisha asilimia 80% ya ajira wanapewa Wazanzibar, Kumbuka Wazanzibar wana kitambulisha cha Mkazi ambacho ndicho utolewa kwa wazawa tu
JE Hii inaweka wapi Muungano wa Tanzania ( Tanganyika Zanzibar ) Je bado tuna Muungano sahihi? ambapo kwenye Muungano huo kuna Mambo mengi yana mkanganyika yanashughulikiwa na nani? na raia wa ili Taifa wana mipaka gani ndani ya Muungano
Masuala ya Ajira kwa upande wa Tanganyika ni ya pande mbili yaani Muungano kwamba ajira zote za Tanganyika zinakwenda kwa mtu yeyote yule, Mfano kuna wakurugenzi wa halmashauri na wakuu wa wilaya wametoka Zanzibar na wako Tanganyika kwa majukumu ya wilaya ambayo yako chini ya TAMISEMI wizara isiyo na mambo ya Muungano. hazi hazikutakiwa kuwa ajira za Muungano maana na mambo ya utumishi wa umma ya upande wa pili, kama ambavyo kwenye mambo ya utumishi wa umma yatokanayo na uteuzi huko Zanzibar kwenye vyeo vya uteuzi wanaopewa ni wazanzibar kwa 100%
Kero zote za sasa zilizopo za Muungano zinatokana na kile ambacho Zanzibar imelalamika, kwa maana nyingine ni Kero za Zanzibar dhidi ya Muungano, lakini hakuna kero za Tanganyika dhidi ya Muungano, Kero tunazoangaika nazo ni za upande mmoja.
Mbaya zaidi Kero hizo zinashughulikiwa na serikali isiyo na uwakilishi wowote wa Tanganyika.
Bado tuna maswali kuhusu uhitaji wa
#KatibaMpya na kuweka vizuri suala la Muungano ? kuwa na serikali Tatu na kila upande kushughulikia mambo yake, Tanganyika kupata uwakilishi kwenye kuondoa kero za Muungano za kutoka Zanzibar na kutoka Tanganyika kupitia Bunge dogo la Muungano litakaloundwa kwenye mfumo wa serikali Tatu ?Zanzibar kuanza kufukuza Watanganyika wanaofanya kazi visiwani upo kwa hoja kwamba si wazawa wa Zanzibar.
Naibu Waziri wa Ajira amesema wakipitisha bajeti, watafanya operesheni inayofanana na ile ya Afrika Kusini kuondoa wasio wazaliwa wa Zanzibar na kuwatendea kazi Wazanzibar bila kuja vigezo vya uzoefu au kitaalumu kuhusu ajira zilizotangazwa. Ameahidi atahakikisha asilimia 80% ya ajira wanapewa Wazawa.
Hii inatia shaka kuhusu Muungano wa Tanzania (Tanganyika Zanzibar). Je, bado tuna Muungano wa kweli?
Masuala ya ajira kwa upande wa Tanganyika ni ya pande mbili: kuna wakurugenzi wa halmashauri na wakuu wa wilaya kutoka Zanzibar waliopo Tanganyika kwa majukumu ya wilaya yaliyoko chini ya TAMISEMI, wizara isiyo na mambo ya Muungano.
Kero za muungano zinatokana na kilicholalamikiwa na Zanzibar; kwa maana nyingine, ni kero za Zanzibar dhidi ya muungano. Hakuna kero za Tanganyika dhidi ya muungano. Kero tunazo nazo ni za upande mmoja.
Mbaya zaidi, kero hizo zinashughulikiwa na serikali isiyo na uwakilishi wowote wa Tanganyika.
Bado tuna maswali kuhusu uhitaji wa
#KatibaMpya na kuweka wazi suala la muungano: kuwa na serikali tatu na kila upande kushughulikia mambo yake, na Tanganyika kupata uwakilishi wa kuondoa kero za muungano zinazotoka Zanzibar na Tanganyika kupitia Bunge dogo la muungano litakaloundwa kwenye mfumo wa serikali tatu.