“Unaonekana/Unaambatana na Nani?”
Kuna “Leverage” kubwa ambayo unaweza kupata kupitia “Credibility” ya watu wengine.
Kuna Broo mmoja ni Mwanasheria, alipomaliza Law School pale Simu 2000, maisha yake yalikuwa magumu kichizi.
Alifungua ofisi yake Tegeta, but kupata wateja ilikuwa kimbembe.
Katika harakati za hapa na pale akabahatika kukutana na ‘Senior Counsel’ ambaye ana uzoefu na ‘Credibility’ kubwa kwenye industry.
Akamwomba awe Mentor wake. Bahati nzuri ‘Senior Counsel’ akakubali.
Appointment ya kwanza walikutana restaurant tu maeneo ya mjini na kupiga msosi.
Appointment ya pili, Mentor alimvutia tu waya akamwambia, “Wiki ijayo twende Mahakamani Kisutu kuna kesi moja ambayo nataka unisaidie kuchukua dondoo za rejea jinsi itakavyoenda”.
Jamaa bila kusita akaenda, na akafanya kama ambavyo Mentor alimwambia.
Siku zilifouata jamaa akawa anaendelea kuambatana na Mentor wake kushiriki kesi za hapa na pale na kupata msosi na social life siku kadhaa za Wikiendi.
LAKINI, jamaa akawa anajiuliza tu kichwani, ‘Mbona Senior hanipi kesi wala haniunganishi na wateja direct’.
Akawa na wasi wasi kidogo. LAKINI, baada ya miezi kadhaa simu zikaanza kuita, “Hallo, Wewe ndiyo......tunakuonaga na Wakili XYZ?”
Pia, Mentor wake akaanza kupokea simu, “Kuna kesi XYZ, in case ratiba yako imejaa, tuunganishe na yule dogo tunayekuonaga naye”.
Kuanzia hapo, jamaa akawa ameshatoboa. Sasa hivi ni Wakili maarufu sana mjini na anawaidia watu wengi sana katika kesi mbalimbali. Siyo hivyo tu, ofisi yake pia imetengeneza nafasi za ajira kwa vijana wengine.
Tunajifunza Nini kupitia Broo;
‘Credibility’ ya watu wengine ni ‘Leverage’ yenye nguvu sana.
>Kuna watu wakikupa ‘Access’ ya kuambatana au kuwa nao karibu wanakugawia ‘Trust’ yao ya watu kwako. Mfano, huyu jamaa yuko na Kibatala siku hizi, basi atakuwa yuko vizuri.
>Kuna watu hawatakupa pesa kutatua shida zako za Leo, lakini watakufungulia mlango wa fursa itakayokusaidia kupata pesa ya kutatua shida zako za kila siku.
>Daima, unapoona kuna uwezekana wa kupata ‘Leverage’ kutoka kwa watu wengine iwe ni kupitia Platform, Associations, mafanikio au kufeli kwao, Mentorship, Referrals, nakadhalika - Aisee ‘Grab it’.
> Usiteseke ku-build kuanzia sifuri kama kuna mtu anaweza kukusogeza ukaanzia kwenye 1 au 2.
NB: Kuwa makini sana usimwangushe aliyekuadhaminisha ‘Credibility’ yake.
Above all, Ukisaidiwa kusimama, na wewe saidia wengine.
All the best.
NB: Ni-follow
@EdwinMjeru ili tuendelee kujifunza kupitia mada mbalimbali kama nilivyoanisha kwenye pinned post.
RT.
EFM.