#JoinTheChain ilikuwa ni kampeni Maalum iliyofanywa na
@ChademaTz kukusanya fedha kwa ajili ya uendeshaji wa Chama kati ya mwezi Februari mpaka Mei 2022.
Kwa wakati huo kipaumbele cha kwanza ilikuwa ni kugharamia Mkutano wa Baraza Kuu 2022 ambalo pamoja na agenda nyingine lilisikiliza rufaa za
#Wasaliti19 waliofukuzwa uanachama. Baada ya hapo fedha za ziada zingetumika kwenye operesheni za Chama ikiwemo za madai ya
#KatibaMpya .
Fedha ambazo Makao Makuu tulipokea kupitia akaunti ya benki na nambari za simu tulizotangaza hapo chini wakati huo zilikuwa shilingi milioni 114. Fedha hizo ziligharamia sehemu ya gharama za Mkutano wa Baraza Kuu la Chama la Mei 2022.
Aidha, pamoja na fedha taslimu kampeni hiyo iliunganishwa pia na ulipaji wa ada na kadi kidigitali ambapo mapato yote kwa ujumla yalikuwa shilingi milioni 371.
Taarifa ya kiwango cha makusanyo na matumizi ilitolewa kwa Kamati Kuu katika vikao vitatu tofauti kwa nyakati mbalimbali hivyo hakuna mjumbe wa Kamati Kuu anayepaswa kusema hafahamu. Majibu sahihi yanapaswa kuwa ama mjumbe hana mamlaka ya kusemea masuala ya fedha au amesahau takwimu.
Nimelazimika kuandika kuhusu suala hili kwa kuwa naona limejirudia rudia mitandaoni na kwenye vyombo vya habari lakini mara zote ambazo Katibu Mkuu nimefanya press conferences halijawahi kuulizwa. Mahesabu ya mwaka husika wa fedha ikiwemo yaliyohusu mapato na matumizi kutoka kampeni
#JoinTheChain yalikaguliwa na Mkaguzi wa Mahesabu (CAG) na Chama kikapata hati safi.
#StrongerTogether #mkutanomkuuchadema2025