Serikali, chini ya
@TIE_Tanzania imefanya kazi kubwa na nzuri ya kupitia upya mitaala ya Elimu kwa ngazi za msingi, sekondari na elimu ya ualimu. Mchakato umekuwa jumuishi na shirikishi kwa lengo la kuboresha maudhui kuyafanya yaendane mazingira ya sasa na pia kutazama upya mbinu za ufundishaji.
Sambamba na hilo, vyuo vikuu chini ya usimamizi wa
@wizara_elimuTz vimelazimika kupitia upya mitaala yake kuakisi mahitaji ya nchi na soko la ajira na kazi. Inatarajiwa kuwa matokeo ya mabadiliko haya makubwa yataanza kuonekana ndani ya miaka michache.