Kutoka katika soko la Kariakoo Jijini Dar es saalaam leo June 24,2024, Wafanyabiashara katika soko hilo wamegoma kufungua maduka yao kwa kile wanachodai ni kutokana na kero wanazokumbana nazo kutoka TRA ikiwemo kurejea kwa kikosi kazi cha kukusanya kodi na kubambikiwa kodi.
@AyoTV_ imepita kwenye Mitaa mbalimbali ya Kariakoo na kuona Wafanyabiashara katika eneo hilo wakiwa wamekaa nje, huku maduka yao yakiwa yamefungwa.
Biashara pekee inayoendelea ni ile inayofanywa na Wafanyabiashara ndogondogo (Machinga) katika Mitaa mbalimbali japo nao wao mgomo huu umewaathiri kwa kile wanachodai kukosa maduka ya kununua bidhaa.
#MillardAyoUPDATES