HOYCE TEMU; MLIMBWENDE MWENYE MAFANIKIO MAKUBWA KULIKO WOTE WALIOPATA KUSHIRIKI SHINDANO LA MISS TANZANIA
(ππΆπ΅π°π¬π’ ππ¬πΆπ΅π’π―πͺ π¬πΈπ’ ππ―π¬π’ππͺ
@issamichuzi π¬πΆπ±πͺπ΅πͺπ’ πΆπ΄π©π°π³π°π£π’ πΈπ’
#ππ’π¬πͺπ―πͺπ¬πͺπ’π π’ππ’π£π’π³πͺ )
Pichani anaonekana Miss Tanzania 1999 Hoyce Temu akiingizwa kama malkia katika ukumbi wa Billicanas jijini Dar es salaam katika hafla maalumu ya kusherehekea ushindi wake iliyohudhuriwa na mama ya mashabiki.
Hapo, Hoyce akiwa na umri wa miaka 21, aliwakilisha chi katika shindano la Miss World lililofanyika Uingereza baadaye mwaka huo.
Hoyce Anderson Temu, mwanadiplomasia, mwandishi wa habari na mtaalamu wa mahusiano ya umma ndiye mlimbwende mwenye mafanikio kuliko wote walioshiriki mashindano ya rembo ya Miss Tanzania tokea yaibuke tena mwaka 1994 baada ya kupigwa marufuku mwaka 1967.
Hii ilidhihirika pale alipoteuliwa kuwa Balozi na kuwa naibu mkuu wa ubalozi katika Ubalozi wa Tanzania huko Geneva, Uswisi, mnamo Mei 23, 2021.
Alipoteuliwa kuwa balozi, tayari alikuwa msomi na mwenye uzoefu wa kitaalamu, katika mahusiano ya umma, uandishi wa habari na mawasiliano. Waajiri wake wa zamani ni pamoja na Standard Chartered Bank, Umoja wa Mataifa na Serikali ya Tanzania.
Alihudumu kama Afisa wa Mahusiano ya Umma katika Shirika la Chakula na Kilimo (FAO), nchini Tanzania mnamo 1999. Kisha alihudumu kwa miaka mitatu iliyofuata kama Katibu wa Kamati ya Telefood ambayo walezi wake walikuwa Rais wa awamu ya tatu marehemu Benjamin Mkapa na mkewe, mama Anna Mkapa.
Hoyce pia alihudumu kama mtangazaji wa televisheni katika kipindi hicho, ambapo wakati mwingine alitumia pesa zake mwenyewe, wakati mwingine michango na wakati mwingine udhamini wa mashirika. Kipindi cha televisheni kiliitwa Mimi na Tanzania ambacho kilisaidia watu wengi sana.
πΈ:
@issamichuzi
@HoyceTemu @MichuziJr @othmanmichuzi @MichuziBlog